Jumanne, 30 Septemba 2014

HAPATOSHI LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA LEO JUMANNE

KIVUMBI kuendelea tena leo na kesho katika ligi ya mabingwa makundi mbalimbali kujaribu bahati zao na kutumia vizuri viwanja vya  nyumbani, mechi ya mapema itaanza majira ya saa moja usiku katika jiji la Moscow nchin Urusi kati ya mabingwa CSKA MOSCOW watavaana na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich.

Majira ya saa tatu na dakika arobaini na tano usiku makundi ya E na H yatawasha moto wakati wenyeji Manchester City wanawakarisha wageni As Roma toka Italia.

Macho na masikio yatakuwa kundi F katika jiji la Paris nchini Ufaransa mabingwa wa ligi hiyo Paris Saint Germain watakuwa wenyeji wa Fc Barcelona toka nchini Hispania kwani timu hizo zimekuwa na upinzani mkubwa kwani hata msimu uliopita  zilikuwa kundi moja ambapo mechi ya kwanza zilitoka sare na ziliporejeana Barcelona walishinda.
  Pia kutakuwa na mechi nyingine katika kundi hilo Apoel Nicosia na Ajax watavaana.

Vijana wa kupaki basi watakuwa nchini Ureno watakumbana na wenyeji  Sporting Lisbon timu ambayo haijafungwa katika mechi zake za ligi sawa na Chelsea nao hawajafungwa katika ligi ya England na Schalke 04 watawapokea Maribor katika kundi hilo la G.

Hitimisho la leo kundi H, Bate Borisov na Athletic Bilbao pamoja na Shakhtar Donetsk vs Fc Porto.

Jumatatu, 29 Septemba 2014

MZIMU WA MSOTI WAENDELEA KUITESA SIMBA

TIMU ya Simba imeendelea kupata sare ya pili mfululizo katika mechi za ligi ya Vodacom Tanzania Bara huku tukiona uwezo wa kila mchezaji anayepata nafasi katika kikosi cha kwanza kati ya wachezaji wote waliosajiliwa na timu hiyo.

Licha ya kuwa na wachezaji wenye viwango vya kimatifa na wenye uzoefu katika mashindano mbalimbali hatujaona makali yao kama vile, kurejea kwa kiungo mkabaji Jonas Mkude hatujaona msaada mkubwa kuwalinda mabeki wake kwani timu hiyo inakosa pumzi katika kipindi cha pili.

Tatizo kubwa ambalo ni changamoto kwa kocha Patriki Phiri na bechi lake la ufundi ni sehemu ya mabeki wake kwani kumekuwa hakuna uwiano mzuri kati ya beki wa mwisho na wa nyuma bado kuna leta shida sana katika ukabaji wake,je nani tumlaum kocha aliyemuacha Donald Musoti ama kamati ya usajili iliyoamua kumsajili Emanueli Okwi?

Kwa upande wangu mzimu wa Musoti utaendelea kuitesa timu hiyo, kwani  ndio alikuwa nguzo imara katika ulinzi akisaidiana na Josefu Owino katika msimu uliopita, ushirikiano wao ulionekana hasa kwenye mechi ya mtani jembe walivyoweza kuwadhibiti washambuliaji wa timu ya Yanga

 Je kulikuwa na haja gani ya kumuacha beki kisiki na kuamua kumrudisha Okwi? ama ndio soka la Usimba na Uyanga wa kukomoana katika suala zima la usajili, wa timu hizi mbili zenye washabiki wengi nchini,ama siasa nyingi na majingambo mengi ambayo hayasaidii katika kujenga timu.

Musoti ni beki wa kimataifa na ana uwezo mkubwa sana katika ukabaji leo hii anaachwa na hatukuona nafasi yake anasajiliwa beki mzoefu  kwa lengo la kuziba nafasi yake. Isihaka bado hajawa na uzoefu katika mikikimiki ya mechi mbalimbali, wadau wengi bado wanajiuliza maswali je ni kocha hakuridhika na kiwango cha mchezaji huyo ama kamati ya usajili kwa ajili ya kufurahisha mashabiki wake na uongozi mpya uliopo sasa?


Ijumaa, 26 Septemba 2014

NANI KUNUNA AMA KUCHEKA WIKIEDI HII MECHI MBALIMBALI BARANI ULAYA?

WIKI hii kuna mechi katika ligi mbalimbali tazama ratiba

LIGI YA ENGLAND

Jumamosi;27
Liverpool               vs       Everton
Chersea                 vs      Aston Villa
Crystal Place          vs      Leicester City
Hull City                 vs     Manchester City
Manchester United  vs  West Ham United
Southampton           vs      Queens Park Rangers
Sunderland               vs     Swansea  City
Arsenal                     vs     Tottenham Hostspur

Jumapili ;28
West Bronwich Albion   vs  Burnely

SERIE A
Jumamosi;27

  Roma           vs            Hellas Veron
  Atalanta        vs           Juventus

Jumapili;28
  Sasoulo             vs        Ssc Napoll
  Cesena              vs         Ac Milan 
 Chievo Veron      vs       Empoll
Inter Milan            vs      Cagllari
Torino                   vs         Fiorentina
Genoa                   vs     Sampdoria

HISPANIA; LIGA BBVA
Ijumaa ;26

Elche     vs   Celta Vigo

Jumamosi;27

Villarreal             vs    Real Madrid
Barcelona           vs    Granada
Athletic Bilbao    vs     Eibar
Atletico Madrid  vs     Sevilla
Levante              vs     Rayo Vallecano

Jumapili;28
Getafe                              vs    Malaga
Deportivo la Coruna         vs     Almeria
Real Sociedad                  vs   Valencia
Cordoba                           vs    Espanyol

UJERUMAN;BUNDESLIGA
Ijumaa;26
Mainz 05     vs    Hoffenham

Jumamosi;27
Fc Cologne            vs          Bayen Munich
Freiburg                 vs          Bayen Leverkusen
Paderborn              vs          Borusia Monchengladbach
Schake 04             vs           Borusia Dotmund
Vfb Sstuttgat          vs           Hannover 96
Wolfsburg              vs           Werder Bremen

Jumapili;28
Augsburg      vs    Hertha Berlin
Hamburger    vs    Eintractfut

UFARANCE;LIGUE 1
 Jumamosi;27
Monaco         vs    Nice
Toulouse         vs    Paris Saint Germain
Lille                vs      Bastia
Lorient            vs    Evian Thonon Gaillard
Metz               vs    Reims
Montpellier      vs  Guingamp

Jumapili;28
Bordeaux      vs    Rennes
Lens              vs   Caen
Nantes           vs   Lyon
Marselle         vs   Saint Etienne

URENO;LIGA ZON SAGRES

Ijumaa;26
Sporting Cp            vs              Fc Port

Jumamosi;27
Estoril            vs                   Benfica
Braga             vs                   Rio Ave


Alhamisi, 25 Septemba 2014

SIMBA YAANDAMWA NA MAJERUHI

KLABU ya simba imeendelea kuandamwa na majeruhi  kuelekea kwenye mchezo wake dhidi ya Polisi Morogoro utakaofanyika Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salam majira ya saa kumi jioni.

Miongoni mwa wachezaji wa timu hiyo ambao wamepata majeruhi ni Issa Rashid ''Baba ubaya'', Paulo Kiongera, Abdi Banda, Nassor Masoud chollo  pamoja na mlinda mlango namba moja Ivo Mapunda.

Licha ya kuwa na majeruhi mengi hatutaraji kuona mapungufu mengi katika timu hiyo kwani ina wachezaji wengi wenye uwezo wa kuziba mapengo hayo, hivyo jukumu kubwa linabaki kwa kocha wa timu hiyo pamoja benchi zima la ufundi kushauriana nani acheze katika nafasi hizo.

Tuliona katika mechi ya ufunguzi timu hiyo ilivyopoteza nafasi nyingi katika sehemu la umaliziaji kwani walikosa nafasi nyingi za kufunga magoli licha ya kuwa na safu hatari ya wafungaji huku ikiongozwa na mfungaji bora wa msimu uliopita Hamis Tambwe raia wa Burundi.

Habari njema kwa mashabiki klabu hiyo ni kurejea kwa kiungo mkabaji Jonas Mkunde aliye kuwa kwenye majeruhi kwa muda mrefu aliyopata akiwa katika kambi ya timu ya Taifa, hivyo ataongeza nguvu katika eneo la kati huku akisaidiana na mabeki wake.

Kwani katika mchezo uliopita tuliona mapungufu katika kiungo mkabaji hasa katika kipindi cha pili mpaka ikapelekea wapinzani kusawazisha magoli yote mawili licha ya kuongoza kipindi cha kwanza.

Jumatano, 24 Septemba 2014

TAZAMA YALIYOJILI LIGI MBALIMBALI KATIKATI YA WIKI HII

Michezo mbalimbali imechezwa wiki hii kutoka ligi tofauti tukianzia;

ENGLAND; CAPITAL ONE

Arsenal             1-2   Southampton
Cardiff city       0-3   B'mouth
Derby county   2-0  Reading
MK Dons         2-0   Bradford
Swansea           3-0  Everton
Sunderland       1-2  Stoke city
Leyton              0-1  Sheffield
Liverpool         2-2  Mid'brough

Shrewsbury     1-0   Norwich city
Fulham            2-1   Doncaster

HISPANIA :LA LIGA

Real Madrid   5-1 Elche
Celta Vigo      2-1 Diportivo la Coruna

ITALIA:  SERIE A

Empoll    2-2   Ac Millan

UJERUMANI: BUNDESLIGA

Bayern munich    4-0 Paderborn
Eintr. Frankfurt    2-2 Mainz 05
Hoffenheim         3-3 Freiburg
Werder Bremen   0-3 Schalke 04

 UFARANSA:  LIGUE 1

Reims         0-5 Marselile
Rennes       0-3 Toulouse

Jumatatu, 22 Septemba 2014

ANGALIA RATIBA YA KOMBE LA LIGI UINGEREZA 'CAPITAL ONE'


Jumanne 23:saa 3:45 usiku

Arsenal       vs    Southmpton
Cardiff        vs    B' mouth
Derby          vs   Reading
Mk Dons     vs   Bradford
Swansea       vs  Everton
Sunderland   vs  Stoke City
Leyton          vs  Sheffield
Liverpool      vs  Mid'brough
Shrewsbury   vs  Norwich city
Fulham          vs   Doncaster

RATIBA ZA LIGI YA BUNDESLIGA,SERIA A NA LALIGA KWA WIKI HII

BUNDESLIGA

Jumanne 23:
Bayern Munich        vs    Paderborn
Eintrach Frankfurt    vs   Mainz 05
Hoffenheim               vs   Freiburg
Werder Bremen         vs   Schalk 04

Jumatano 24:
Bayer Leverkusen                 vs  Augsburg
Borrusi Dortmund                 vs  Vfb Stuttgat
Borrusia monchengladbach   vs  Hamburger sv
Hannover 96vs                       vs  Fc cologne
Hertha Berlin                         vs  Wolfsburg

LA LIGA

Jumatatu 22:
Getafe        vs    Valencia

Jumanne 23:
 Real Madrid    vs  Elche
Celta vigo         vs  Deportivo la coruna

Jumatano 24:
Almeria             vs  Atletico Madrid
Eibar                  vs  Villarreal
Rayo vallecano  vs  Athletic Bilbao
Granad                vs  Levante
Malaga                vs  Barcelona
Sevilla                 vs  Real sociedad

SERIA A

Jumanne 23:
Empoll       vs  Ac millan

Jumatano 24:
Calgllarl          vs    Torino
Fiorentina        vs   Sassuolo
Hellas verona   vs   Genoa
Inter millan       vs  Atalanta
Juventus            vs   Cesena
Parma                vs   Roma
Ssc Napoll          vs  Palermo
Sampdoria           vs Chievo verona

Alhamis 25:
Lazio         vs     Udenese