Jumamosi, 4 Oktoba 2014

YANGA KUIBANA MBAVU RUVU JKT UWANJA WA TAIFA


MAKALI ya timu ya Yanga kuendelea kwa wanajeshi Jkt Ruvu katika mzunguko wa tatu wa ligi ya Vodacom Tanzania bara. Huku kila timu ikitafuta point tatu muhimu huku vijana wa Fred Minziro wakitafuta ushindi wa kwanza kwani wametoka sare moja dhidi ya Mbeya City pamoja na kufungwa na mabingwa watetezi Azam Fc.

Hivyo kwa siku ya kesho tutaona mechi itakuwa ngumu kwa pande zote mbili,  Yanga iliyo chini ya kocha Mbrazil Marcio Maximo ikitaka kuendeleza ushindi wa pili baada ya kuifunga Tanzania Prisons kwani mechi ya kwanza walifungwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro magoli mawili kwa bila katika uwanja wa Jamhuri.

Je Andrey Coutinho ataendelea kuwatesa mabeki wa timu pinzani?  kwani tuliona katika mechi yake ya kwanza ya ligi alionyesha kazi na ufundi wa kuuchezea mpira, hali iliyopelekea kufunga goli zuri kwa njia ya faulo huku akiwa ametoka kwenye majeruhi yaliyomfanya akose mechi ya ufunguzi.

Hata hivyo upinzani utakuwa mkali kwa kuwa kocha Minziro anawafahamu vizuri Yanga alishawahi kuwafundisha Yanga,  swali la kujiuliza atakubali kufungwa na Maximo ama atapeleka msiba jangwani?  hilo ni swali ambalo kitendawili kitajibiwa  katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salamu.

Kwa kawaida mabeki wa Jkt Ruvu watakuwa na kazi ngumu kwani timu ya Yanga ina washambuliaji,viungo pamoja na mawinga wenye kasi  akili yakupiga mipira mifupi mifupi. Hivyo Ruvu wataingia kwa kukamia mechi wakitambua wazi kuwa watakutana na aina ya wachezaji wajanjahali itakayowaathiri kama ilivyokuwa kwa Prisons 

Kasi, nguvu na akili za winga machachari  Mrisho Ngasa,Simoni Msuva pamoja na wabrazil Coutinho na Jaja zinaweza kutosha kupeleka msiba mkubwa kwa Ruvu JKT wasipotambua nini wanapaswa kukifanya kwa wanajangwani hao.

RATIBA YA LIGI KUU MAARUFU ZOTE DUNIANI WIKIENDI HII




LIGI KUU ENGLAND

Hull city             vs  Crystal Palace

Leicester City   vs   Burnely

Liverpool           vs  West Bromwich Albion

Sunderland       vs  Stoke City

Swansea City     vs  Newcastle United

Aston Villa         vs   ManchesterCity


ITALIA; SERIE A

Hellas Verona  vs  Cagliari

Ac Milan            vs    Chievo Verona

HISPANIA;LIGA BBVA.

Valencia                 vs    Atletico Madrid
Rayo Vallecano   vs     Barcelona
Eibar                        vs     Levante
Almeria                  vs     Elche
Malaga                    vs     Granada


UJERUMANI;BUNDESLIGA.

Bayer Leverkusen        vs   Paderborn
Bayern Munich             vs   Hannover 96
Borrusia Dortmund    vs  Hamburger Sv
Hoffenheim                    vs  Schalke 04
Werder Bremen            vs  Freiburg
Eintracht.Frankfurt   vs  Fc Cologne

UFARANSA;LIGUE 1

Caen             vs   Marseille
Bastia          vs   Lorient
Evian T G   vs   Metz
Nice              vs   Montpellier
Rennes        vs   Lens

Alhamisi, 2 Oktoba 2014

ARSENAL BILA KUPEPESA MACHO WAPELEKA MSIBA MZITO UTURUKI.



WASHIKA,bunduki wa Jiji la Kaskazini mwa London timu ya Arsenal kuamkia usiku wa Ulaya jana wamefanya mauaji makubwa dhidi ya wahuni wa Uturuki timu ya Galatasaray kwa kuwafunga magoli manne kwa moja.

 Iliwachukua dakika ya ishirini na mbili kipindi cha kwanza mshambuliaji hatari aliye sajiliwa  katika  dakika za majeruhi toka kwa wapinzani wao Manchester United Dany Welback aliipatia goli la kwa baada ya kupokea pasi zuri toka kwa Alexis Sanchez ,dakika 30 aliweka nyavuni goli la pili safari hii akiwahi pasi ya Mesut Ozil kabla ya kwenda mapumziko Alexis Sanchez alihitimisha goli la tatu.

Kipindi cha pili kilianza kwa kushambuliana kwa zamu huku wageni wakitafuta kurejesha magoli yote waliofungwa kipindi cha kwanza dakika ya hamsini Welback aliandika hat trick yake ya kwanza akiwa na Arsenal na pia ni goli lake la nne tangu ajiunge na timu hiyo.

Mshambuliaji huyo aliyekuwa mwiba kwa kuisumbua ngome ya wapinzani hao huku Felipe Melo akizungushwa na Sanchez pamoja  mabeki wake dakika ya 69 washika bunduki hao walipata pigo baada ya mlinda mlango Szczesny kupata kandi nyekundu kwa kosa la kumdaka mshambuliaji  wa Galatasaray.

Jumatano, 1 Oktoba 2014

ARSENAL NA MAJERUHI KUWAVAA WATURUKI LEO HII

PATASHIKA ya ligi ya mabingwa kuendelea leo hii baada ya kushudia vigogo toka Hispania timu ya Barcelona wakichezea kichapo cha magoli matatu toka kwa mabingwa wa Ufaransa timu ya Paris Saint Germain, Chelsea, Bayern Munich,wakipata ushindi wa ugenini na pia Manchester City wameendelea kuchechemea baada ya kulazimishwa sare na Roma toka Italia.

Je nani kuibeba Arsenal kwani kila siku majeruhi wanaongezeka baada ya kuona viungo wa timu hiyo kama Mikel Arteta, Aron Ramsey, Jack Wilshere watakosa mechi ya leo dhidi ya timu ya Galatasaray toka nchini Uturuki.Hivyo jukumu la kiungo mkabaji itawategemea Flamini, Diaby,Rosicky nani ataanza katika kikosi cha kwanza.


Hivyo kutakuwa na mabadiliko kwani namba nane atasimama Alex Oxlade-Chamberlain kulia na kushoto Mesut Ozil na Alexis Sanchez wataongoza kutoa pasi kwa Santi Cazorla na Dany Welbeck huu utakuwa mtihani mgumu kwa Asener Wenger kwani mwishoni mwa wiki atakuwa ugenini kupepetana na watoto wa kupaki basi Chelsea ambao mpaka sasa hawajafungwa katika ligi ya England .

Mechi nyingine
Atletico Madrid vs Juventus,
Fc Basel             vs Liverpool
Malmo               vs  Real Madrid


Jumanne, 30 Septemba 2014

HAPATOSHI LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA LEO JUMANNE

KIVUMBI kuendelea tena leo na kesho katika ligi ya mabingwa makundi mbalimbali kujaribu bahati zao na kutumia vizuri viwanja vya  nyumbani, mechi ya mapema itaanza majira ya saa moja usiku katika jiji la Moscow nchin Urusi kati ya mabingwa CSKA MOSCOW watavaana na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich.

Majira ya saa tatu na dakika arobaini na tano usiku makundi ya E na H yatawasha moto wakati wenyeji Manchester City wanawakarisha wageni As Roma toka Italia.

Macho na masikio yatakuwa kundi F katika jiji la Paris nchini Ufaransa mabingwa wa ligi hiyo Paris Saint Germain watakuwa wenyeji wa Fc Barcelona toka nchini Hispania kwani timu hizo zimekuwa na upinzani mkubwa kwani hata msimu uliopita  zilikuwa kundi moja ambapo mechi ya kwanza zilitoka sare na ziliporejeana Barcelona walishinda.
  Pia kutakuwa na mechi nyingine katika kundi hilo Apoel Nicosia na Ajax watavaana.

Vijana wa kupaki basi watakuwa nchini Ureno watakumbana na wenyeji  Sporting Lisbon timu ambayo haijafungwa katika mechi zake za ligi sawa na Chelsea nao hawajafungwa katika ligi ya England na Schalke 04 watawapokea Maribor katika kundi hilo la G.

Hitimisho la leo kundi H, Bate Borisov na Athletic Bilbao pamoja na Shakhtar Donetsk vs Fc Porto.

Jumatatu, 29 Septemba 2014

MZIMU WA MSOTI WAENDELEA KUITESA SIMBA

TIMU ya Simba imeendelea kupata sare ya pili mfululizo katika mechi za ligi ya Vodacom Tanzania Bara huku tukiona uwezo wa kila mchezaji anayepata nafasi katika kikosi cha kwanza kati ya wachezaji wote waliosajiliwa na timu hiyo.

Licha ya kuwa na wachezaji wenye viwango vya kimatifa na wenye uzoefu katika mashindano mbalimbali hatujaona makali yao kama vile, kurejea kwa kiungo mkabaji Jonas Mkude hatujaona msaada mkubwa kuwalinda mabeki wake kwani timu hiyo inakosa pumzi katika kipindi cha pili.

Tatizo kubwa ambalo ni changamoto kwa kocha Patriki Phiri na bechi lake la ufundi ni sehemu ya mabeki wake kwani kumekuwa hakuna uwiano mzuri kati ya beki wa mwisho na wa nyuma bado kuna leta shida sana katika ukabaji wake,je nani tumlaum kocha aliyemuacha Donald Musoti ama kamati ya usajili iliyoamua kumsajili Emanueli Okwi?

Kwa upande wangu mzimu wa Musoti utaendelea kuitesa timu hiyo, kwani  ndio alikuwa nguzo imara katika ulinzi akisaidiana na Josefu Owino katika msimu uliopita, ushirikiano wao ulionekana hasa kwenye mechi ya mtani jembe walivyoweza kuwadhibiti washambuliaji wa timu ya Yanga

 Je kulikuwa na haja gani ya kumuacha beki kisiki na kuamua kumrudisha Okwi? ama ndio soka la Usimba na Uyanga wa kukomoana katika suala zima la usajili, wa timu hizi mbili zenye washabiki wengi nchini,ama siasa nyingi na majingambo mengi ambayo hayasaidii katika kujenga timu.

Musoti ni beki wa kimataifa na ana uwezo mkubwa sana katika ukabaji leo hii anaachwa na hatukuona nafasi yake anasajiliwa beki mzoefu  kwa lengo la kuziba nafasi yake. Isihaka bado hajawa na uzoefu katika mikikimiki ya mechi mbalimbali, wadau wengi bado wanajiuliza maswali je ni kocha hakuridhika na kiwango cha mchezaji huyo ama kamati ya usajili kwa ajili ya kufurahisha mashabiki wake na uongozi mpya uliopo sasa?


Ijumaa, 26 Septemba 2014

NANI KUNUNA AMA KUCHEKA WIKIEDI HII MECHI MBALIMBALI BARANI ULAYA?

WIKI hii kuna mechi katika ligi mbalimbali tazama ratiba

LIGI YA ENGLAND

Jumamosi;27
Liverpool               vs       Everton
Chersea                 vs      Aston Villa
Crystal Place          vs      Leicester City
Hull City                 vs     Manchester City
Manchester United  vs  West Ham United
Southampton           vs      Queens Park Rangers
Sunderland               vs     Swansea  City
Arsenal                     vs     Tottenham Hostspur

Jumapili ;28
West Bronwich Albion   vs  Burnely

SERIE A
Jumamosi;27

  Roma           vs            Hellas Veron
  Atalanta        vs           Juventus

Jumapili;28
  Sasoulo             vs        Ssc Napoll
  Cesena              vs         Ac Milan 
 Chievo Veron      vs       Empoll
Inter Milan            vs      Cagllari
Torino                   vs         Fiorentina
Genoa                   vs     Sampdoria

HISPANIA; LIGA BBVA
Ijumaa ;26

Elche     vs   Celta Vigo

Jumamosi;27

Villarreal             vs    Real Madrid
Barcelona           vs    Granada
Athletic Bilbao    vs     Eibar
Atletico Madrid  vs     Sevilla
Levante              vs     Rayo Vallecano

Jumapili;28
Getafe                              vs    Malaga
Deportivo la Coruna         vs     Almeria
Real Sociedad                  vs   Valencia
Cordoba                           vs    Espanyol

UJERUMAN;BUNDESLIGA
Ijumaa;26
Mainz 05     vs    Hoffenham

Jumamosi;27
Fc Cologne            vs          Bayen Munich
Freiburg                 vs          Bayen Leverkusen
Paderborn              vs          Borusia Monchengladbach
Schake 04             vs           Borusia Dotmund
Vfb Sstuttgat          vs           Hannover 96
Wolfsburg              vs           Werder Bremen

Jumapili;28
Augsburg      vs    Hertha Berlin
Hamburger    vs    Eintractfut

UFARANCE;LIGUE 1
 Jumamosi;27
Monaco         vs    Nice
Toulouse         vs    Paris Saint Germain
Lille                vs      Bastia
Lorient            vs    Evian Thonon Gaillard
Metz               vs    Reims
Montpellier      vs  Guingamp

Jumapili;28
Bordeaux      vs    Rennes
Lens              vs   Caen
Nantes           vs   Lyon
Marselle         vs   Saint Etienne

URENO;LIGA ZON SAGRES

Ijumaa;26
Sporting Cp            vs              Fc Port

Jumamosi;27
Estoril            vs                   Benfica
Braga             vs                   Rio Ave