Jumatatu, 27 Oktoba 2014

SIMBA SASA HALI YAZIDI KUWA TETE

SARE,ya tano mfululizo katika klabu ya Simba imewachanganya viongozi pamoja na kocha mkuu wa timu hiyo Patrick Phiri na benchi lake la ufundi,  mpaka kufikia hatua ya kuwatuhumu baadhi ya wachezaji wa timu hiyo akiwemo Amri Kiemba na Haruna Chanongo kuwa hawajitumi ipasavyo.

Kwa kawaida matokea ya timu hiyo ni mazuri kwani mpaka sasa haijafungwa katika ligi ya Vodacom Tanzania Bara kufungwa,sare na kupata point ni moja ya matokeo ya mpira wa mguu kwa hali inavyoendelea. Kunaelekea katika timua timua ya kocha,wachezaji kutuhumiwa kuwa wanahujumu timu kwani ndio ilivyo katika klabu zetu kongwe hapa nchini  zenye viongozi walioathirika kimawazo.

Tujiulize nani wa kulaumiwa katika timu hiyo kati ya  wachezaji na kocha? ama uongozi wenyewe ukae chini ujiulize nani mchawi wa sare tano kwa upande wangu naona ndani ya uongozi kuna matatizo,  kuna kundi la Ukawa ambalo limefutwa uanachama kuwa waliipeleka Simba Mahakamani katika kipindi cha Uchaguzi uliopita.

Kwanini nasema kuwa kuna matatizo katika timu hiyo ni kuwa baadhi ya wachezaji wameanza kutuhumiwa kuwa wanahujumu timu kwa mjibu wa kiongozi moja wa timu hiyo,  amefikia hatua ya kusema katika chombo kimoja cha habari kuwa, Amri Ramadhani Kiemba  anahujumu timu kwa kucheza chini ya kiwango akiwa kwenye timu ya Taifa Star anacheza kwa kujituma.?

Kweli kwa hali ilivyo Kiongozi kuanza  kumtuhumu mchezaji kwa kuangalia kocha Phiri hampi nafasi kubwa  ya kucheza na kwenye kikosi chake huku  timu ya Taifa anaaminiwa na kocha mkuu. Sasa kiongozi huyo ana ushahidi gani kuwa mchezaji huyo  anahujumu timu? basi angejaribu japo kutumia busara ya kuzungumza na wachezaji anaowahisi wanaihujumu timu kwanza  au hata kundi linalijiita Ukawa pamoja na Baraza la Wazee wa timu hiyo ambao wanaonekana kutengwa na Uongozi na sio kuwanyoshea kidole wachezaji.

Huo unaonekana kuwa mwanzo tu lakini inawezekana zengwe hili litamkuta  hata kocha mkuu wa  wa timu hiyo kwani baada ya kutoka sare na Prison ya mkoani Mbeya  kuna mambo mengi yatatokea katika timu likiwemo la  kusimamishwa kwa wachezaji kumkalisha kitimoto kocha mkuu na benchi lake la ufundi. Kwa matokeo mabaya yanayoikumba klabu hiyo usije kushangaa kuona Kiemba,Shabani Kisinga na Haruna Chanongo wamesimamishwa kwa kutuhumiwa kwa kuhujumu timu.

Hivyo tunachoomba wana msimbazi waendelee kuwaamini wachezaji na sio kuanza kutuhumu kwa mambo ya siasa kwani tatizo wanalo wenyewe cha kuwashauri wakae chini na Ukawa na Wazee wa klabu hiyo,  ili watatue matatizo ya timu na wala sio kuwalaumu wachezaji. Tunajua kuwa Simba ina Rais anayejua mpira Evans Aveva atumie busara kutatua mgogoro uliopo ndani ya timu maana inavyoelekea mambo yataendelea kuwa magumu kupita maelezo.

itaendelea wiki ijayo


Ijumaa, 24 Oktoba 2014

DUNIA ITASIMAMA KWA DAKIKA 90 USIKU WA EL CLASSICO


DUNIA itasimama kwa muda wa dakika tisini  majira ya saa moja kamili usiku pale mahasimu wa soka nchini Hispania  Barcelona na Real Madrid  katika mechi ya la liga, upinzani uliopewa jina la El Classico na pia zikipambwa na majina makubwa ya wanasoka wenye upinzani mkubwa kwa soka la sasa  Messi na Ronaldo.

Upinzani utaongezeka kwa pande zote mbili kwani kila timu imesajili wachezaji wapya, macho na masikio ni kwa nyota mpya wa timu ya Barcelona Luis Suerez,  kwa mara ya kwanza ataonekana katika timu yake. Baada ya kumaliza kifungo cha miezi minne baada ya kumnga'ta  mchezaji wa timu ya Taifa ya Italia  la katika fainali za kombe la dunia zilizofanyika nchini Brazil.

Kwa upande wa mechi yenyewe itakuwa ngumu kwa kila upande kwani  sasa timu ya Barcelona haijafungwa na pia haijaruhusu goli lolote katika michezo minane ya ligi hiyo na kujikusanyia point ishirini na mbili imeshinda saba na kutoka sare moja. Na mahasimu wao wana point kumi na nane wamefungwa mechi moja na kutoka sare moja.

Macho ya wengi ni kwa wachezaji wa timu hizo Lionel Mess, Christian Ronaldo ndio wanatazamwa kwa kila mtu kutokana na ubora walio nao kwa sasa japo kuwa Ronaldo anaongoza kwa kupachika magoli kwa ligi hiyo ana magoli kumi na tano na mpinzani wake ana magoli saba.

Je Luiz Suerez ataanza vyema kwa timu yake kwa kushirikiana na nyota aliye kwenye kiwango cha juu kwa sasa na ndie anaongoza kwa kupachika magoli katika klabu yake Junior Santos Nermar pingo kubwa litakuwa kwa Real Madrid kwa kumkosa winga wao hatari aliye majeruhi Gareth Bale.

Alhamisi, 23 Oktoba 2014

HATIMAYE REAL MADRID YALIPA KISASI CHA MWAKA 2008 KWA LIVERPOOL

KISASI timu ya Real Madrid toka nchini Hispania usiku wa kuamkia leo imetoka kifua mbele baada ya kulipa kisasi cha mwaka 2008 cha kufungwa magolin manne kwa moja mshambuliaji aliye kwenye kiwango cha Dunia Christian Ronaldo ameendelea kucheka na nyavu za wapinzani baada ya kufungwa goli la kwanza na magoli mawili yakifungwa na Karim Benzema yote yakipatikana kipindi cha kwanza.

Matokeo mengine Atletico Madridi wakiwaangamiza Malmo FC magoli matano kwa bila,huko nchini Uturuki vibonde  Galatasaray wameendelea kugawa point baada ya kufungwa magoli manne kwa bila na vibonde wa ligi ya Ujerumani Borrusia Dotmund ambao mpaka sasa hawajafungwa goli lolote kwenye kundi hilo.

Arsenal wamepata ushindi wao kwa taabu baada ya kuwafunga Anderlecht magoli mawili kwa moja nchini Ufaransa Monaco wakitoka sare ya bila kufungana na Benfica huko kibibi kizee Juventus toka nchini Italia wakipokea kichapo toka kwa Olimpiakos kwa goli moja kwa bila.

MZUNGUKO ROUNDI YA TANO LIGI YA VODACOM TANZANIA BARA KUENDELEA WIKIENDI HII SIMBA NA YANGA UGENINI?

Mzunguko roundi ya tano wa ligi ya  Vodacom Tanzania Bara kuendelea tena mwishoni mwa wiki hii katika viwanja tofauti tofauti macho na masikio ya wengi yatakuwa katika viwanja vya Kambarage mjini Shinyanga na Sokoine mjini Mbeya huku vigogo vya Simba na Yanga vitakuwa ugenini.

Mechi nyingine mabingwa watetezi wa ligi hiyo Azam FC watakuwa nyumbani kuwaalika watoto waliokuwa usingizini Jkt Ruvu katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salamu huku watoto wa Mabati Pwani Ruvu shooting mara baada ya kuzinduka mpaka kupelekea kufukuzwa kwa kocha wa Ndanda FC watakuwa nyumbani kupepetana na Polisi Morogoro,wagonga nyundo Mbeya City baada ya kupokea kichapo toka kwa Azam watakuwa nyumbani kuwapokea vijana toka kwenye mashamba ya Miwa Mtibwa Sugar.

Je Simba atavunja mwiko dhidi ya Tanzania Prison katika uwanja wa Sokoine ambao umekuwa mgumu mno kwa wekundu wa msimbazi mara nyingi tumeshudia wakichezea vichapo ama kutoka sare Simba hawana bahati katika viwanja vya mikoani kwani hata msimu uliopita walipata point tatu tu katika mechi za ugenini nyingi walitoka sare pamoja na kufungwa ushindi wao ulikuwa katka uwanja wa Sheik Abedi Karume mjijini Arusha dhidi ya Jkt Oljoro.

Watoto wa Marcio Maximo watakuwa wageni wa timu mpya iliyo panda ligi kuu kwa mara ya kwanza Stand United ambayo mpaka sasa haijapoteza mechi yeyote ya ugenini kwani imeweza kupata pointi tano japo ilianza vibaya katika uwanja wake wa nyumbani kwa kufungwa magoli manne kwa moja na Ndanda FC,je watakuwa wateja katika uwanja wake dhidi ya timu ya Yanga?

Mara nyingi tumeshudia timu za Simba na Yanga zinapocheza ugenini huwa zinakabiwa mno na timu pinzani kutokana na kuwa na majina makubwa katika soka la Tanzania mambo mengi hutokea katika mechi hizo ushirikina mara nyingi hutokea mfano msimu uliopita mjini Tanga mchezo baina Jkt Mgambo naTimu ya Yanga na Mbeya City na Simba mjini Mbeya mambo hayo ya ushirikina yalitokea katika viwanja vingi ambapo Simba na Yanga zinapokuwa ugenini.

Kwa muda mrefu wakazi wa mjini Shinyanga hawakuwa na timu kwa takribani miaka kumi hawazioni timu za Simba naYanga baada ya timu yao iliposhuka daranja Kahama Unitedi hajawahi tena kuona uwanja wao ukitumika tunajua jumamosi mechi itakuwa kali na kusisimu kwa timu zote mbili na pia uwanja utafurika mno hii kutokana na watu wengi wa kanda ya ziwa kuwa hamasa ya mpira.

Hivyo tunatarajia kuwa mechi yote itakuwa migumu kutokana na kila timu zimejipanga vya kutosha katika safari ya kutafuta pointi tatu muhimu kwa kila timu wasimamzi,wamzi tunawaomba wafate sheria zote za mpira wa miguu hatutaki kuona wakipendelea timu fulani pamoja na timu zitakapofungwa mara nyingi tumeona makocha huwa wanalalamika pindi timu zinapofungwa utasikia refa kapendelea timu fulani ama viwanja vibovu yote hayo hutokea mara tu dakika tisini za mwamuzi zinapoisha.














































































 

Jumatano, 22 Oktoba 2014

JE LIVERPOOL KUENDELEZA UTEJA KWA REAL MADRID AU REAL MADRID KULIPA KISASI LEO HII?

USIKU wa ulaya kuendelea leo hii katika viwanja tofauti tofauti swali la kujiuliza nani atavuna idadi kubwa ya magoli kama mechi za jana kwani magoli 40 yalipatikana huku Bayern Munich na Shakhtar Donestik zikifanya mauaji ya kutosha kwani ziliweza kushinda kwa idadi kubwa ya magoli.

Macho na masikio yatakuwa nchini England majogoo wa Anfield Liverpool watakuwa wanapepetana na mabingwa watetezi wa kombe hilo Real Madrid toka Hispania huo utakuwa mchezo mkali na wa kuvutia kwa  timu zote mbili kwani  zinapokutana huwa zina upinzani mkubwa mno.

Je Liverpool wataendeleza ubabe kwa mabingwa hao ama Madrid watalipa kisasi cha magoli manne waliofungwa katika mechi ya mwisho kukutana mwaka 2008\09 katika mchezo wa kwanza Liverpool alishinda goli moja kwa bila na ziliporejeana kwa mara nyingine Liverpool alishinda magoli manne kwa moja.

Mechi nyingine watoto wa kaskazini mwa London timu ya Arsenal watakuwa ugenini nchini Ubelgiji kupepetana na Anderlecht,Nchini Ufaransa matajiri Monaco wanaochechemea katika ligi ya kwao watawapokea vijana toka Ureno Benfica, vibonde toka Ujerumani Borrusia Dotmund watakuwa ugenini na wahuni wa Uturuki Galastaray,Atletico Madrid watakuwa nyumbani na Malmo FC.

Jumatatu, 6 Oktoba 2014

LIGI  ya Vodacom Tanzania bara ipo katika mzunguko wa tatu tumeshudia timu mbalimbali zikiendeleza ushindi nyingine sare pamoja na kufungwa hayo yote ni matokeo ya mpira kwani kuna kushinda,sare na kufungwa.

Je tutafika katika kukuza mpira wa Tanzania tuwe kama  nchi  nyingine barani Afrika ama Ulaya? kwani mpaka sasa kuna mvutano baina ya TFF na timu zinazoshiriki katika ligi hiyo shirikisho linalosimamia mpira tayari limesema lazima kila timu ikatwe asilimia tano ya wadhamini wa ligi.

Ambao ni Vodacom pamoja na Azam Media kwani ndio wadhamini wa ligi hiyo kwa mjibu wa TFF wamesema wameazisha mfuko wa maendeleo ya timu za vijana na mapato yake yatapatikana kutokana na makato ya vilabu vinavyoshiriki ligi ya Vodacom je huu ni mfumo sahihi kwa shirikisho hilo chini ya Rais Jamal Malinzi vimezingatia hali halisi iliyopo katika timu zinazoungaunga kupata hela?

Kuna haja gani vilabu vikatwe mapato kama hayo kwanini TFF isibuni njia nyingine ya kupata hizo pesa za kuendeshea vijana mpaka isake mapato kwa timu hizo huu ni mgogoro mkubwa mno kwani kila upande ukimtunishia  misuri mwenzake na tayari Malinzi kasema lazima kila timu ikatwe asilimia tano huku mwanasheria wa vilabu hivyo Damasi Ndumbaro amesema haiwezekani kukatwa asilimia hiyo.

Je timu kama Stand United ,Ndanda Fc, Coast Union, ambazo zinapata hela kutoka kwa kutembeza bakuli kwa watu zitaweza kweli kuwalipa mishahara wachezaji na benchi zima la ufundi mpaka leo hii vilabu vinalia pesa haitoshi kwa mahitaji ya timu haki imetendeka ama shirikisho hilo limekurupuka kwa maamuzi hayo kwa vilabu.

Kwa hili naona TFF hawajatenda haki kwa kuamua kuingia kwenye mvutano ambao hauna maana kwa kuendesha mpira wa miguu wangebuni kitu kingine cha kuwaingizia mapato bila wasiwasi mfano mzuri wangeandaa semina kwa wadau wa mpira na pia wangeandaa mechi maalum kwa timu ya Taifa kwa lengo kupata hizo pesa na pia wangetafuta wadhamini.

Kwa ushauri wangu kwa shirikisho hilo liache kutumia nguvu kwa vilabu hivyo bali litumie vyanzo vingine kwa kuendeshea mfuko huu ambao wameanzisha na sio kwa kuzizamisha timu mpaka ikapelekea kuvurungika kwa ligi hiyo, maana tunapoelekea mambo mengi yataendelea kutokea.

Hivyo busara itumike kwa maamuzi hayo hatupendi kuona soka letu likiendelea kuwa chini badala ya kufikiri mbele kwani sisi tunazozana na makato ya pesa wenzetu wanafikiria maandalizi ya kombe la Dunia mwaka 2018 litakalo fanyika nchini Urusi.

















Jumamosi, 4 Oktoba 2014

MASIKINI SIMBA AKOSA NYAMA KAOKOTEZA MAJANI

LIGI kuu ya Vodacom Tanzania bara imeendelea tena wikiendi hii huku michezo kadhaa ikipigwa katika viwanja vitano tofauti lakini kubwa zaidi ni ile mechi kati ya Simba na Stand United iliyochezwa uwanja wa taifa  Dar Es Salaam ikishuhudiwa Simba ikilazimishwa tena sare ya goli moja kwa moja.

Hii ni sare ya tatu kwa timu ya Simba tangu ligi kuu ianze na hivyo imepata pointi tatu na magoli manne katika michezo mitatu walioicheza tena katika uwanja mmoja wa taifa,  hali inayoonesha kuwa bado haijajipanga vizuri kukabiliana na mikikimikiki ya ligi kuu inayoonekana kuwa ngumu kwa timu zote kucheza kwa juhudi kuhakikisha wanavuna pointi tatu muhimu ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kuwania kombe hilo.

Kuna mambo ambayo huibuka pindi hizi timu kongwe kama Simba inapozidiwa na kutoa matokeo ya aina kama hii kuwa inawezekana kuna tatizo, huku wakisahau kuwa mchezo ni mabadiliko na kila timu inafanya jitihada kubwa kuhakikisha inavuna pointi tatu. Hivyo matokeo wanayoyapata ni ya kawaida sana kutokana na ukweli kuwa kwa sasa dunia imebadilika na kila timu imebadilika na inafanya kila mbinu kuhakikisha wanapata matokeo mazuri.

Hivyo ni bora wapenzi na wadau wa soka wakaelewa kuwa mpira hausimami katika umbo lilelile bali hubadilika kulingana na wakati na namna dunia inavyoendelea, kinachotakiwa kwa timu ya simba ni kuhakikisha wanabaini nini kinawakwamisha kupata ushindi ili kujikwamnua na hali hii inayoonekana kuwakatisha tamaa mashabiki wa timu hiyo


YANGA KUIBANA MBAVU RUVU JKT UWANJA WA TAIFA


MAKALI ya timu ya Yanga kuendelea kwa wanajeshi Jkt Ruvu katika mzunguko wa tatu wa ligi ya Vodacom Tanzania bara. Huku kila timu ikitafuta point tatu muhimu huku vijana wa Fred Minziro wakitafuta ushindi wa kwanza kwani wametoka sare moja dhidi ya Mbeya City pamoja na kufungwa na mabingwa watetezi Azam Fc.

Hivyo kwa siku ya kesho tutaona mechi itakuwa ngumu kwa pande zote mbili,  Yanga iliyo chini ya kocha Mbrazil Marcio Maximo ikitaka kuendeleza ushindi wa pili baada ya kuifunga Tanzania Prisons kwani mechi ya kwanza walifungwa na Mtibwa Sugar ya Morogoro magoli mawili kwa bila katika uwanja wa Jamhuri.

Je Andrey Coutinho ataendelea kuwatesa mabeki wa timu pinzani?  kwani tuliona katika mechi yake ya kwanza ya ligi alionyesha kazi na ufundi wa kuuchezea mpira, hali iliyopelekea kufunga goli zuri kwa njia ya faulo huku akiwa ametoka kwenye majeruhi yaliyomfanya akose mechi ya ufunguzi.

Hata hivyo upinzani utakuwa mkali kwa kuwa kocha Minziro anawafahamu vizuri Yanga alishawahi kuwafundisha Yanga,  swali la kujiuliza atakubali kufungwa na Maximo ama atapeleka msiba jangwani?  hilo ni swali ambalo kitendawili kitajibiwa  katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salamu.

Kwa kawaida mabeki wa Jkt Ruvu watakuwa na kazi ngumu kwani timu ya Yanga ina washambuliaji,viungo pamoja na mawinga wenye kasi  akili yakupiga mipira mifupi mifupi. Hivyo Ruvu wataingia kwa kukamia mechi wakitambua wazi kuwa watakutana na aina ya wachezaji wajanjahali itakayowaathiri kama ilivyokuwa kwa Prisons 

Kasi, nguvu na akili za winga machachari  Mrisho Ngasa,Simoni Msuva pamoja na wabrazil Coutinho na Jaja zinaweza kutosha kupeleka msiba mkubwa kwa Ruvu JKT wasipotambua nini wanapaswa kukifanya kwa wanajangwani hao.

RATIBA YA LIGI KUU MAARUFU ZOTE DUNIANI WIKIENDI HII




LIGI KUU ENGLAND

Hull city             vs  Crystal Palace

Leicester City   vs   Burnely

Liverpool           vs  West Bromwich Albion

Sunderland       vs  Stoke City

Swansea City     vs  Newcastle United

Aston Villa         vs   ManchesterCity


ITALIA; SERIE A

Hellas Verona  vs  Cagliari

Ac Milan            vs    Chievo Verona

HISPANIA;LIGA BBVA.

Valencia                 vs    Atletico Madrid
Rayo Vallecano   vs     Barcelona
Eibar                        vs     Levante
Almeria                  vs     Elche
Malaga                    vs     Granada


UJERUMANI;BUNDESLIGA.

Bayer Leverkusen        vs   Paderborn
Bayern Munich             vs   Hannover 96
Borrusia Dortmund    vs  Hamburger Sv
Hoffenheim                    vs  Schalke 04
Werder Bremen            vs  Freiburg
Eintracht.Frankfurt   vs  Fc Cologne

UFARANSA;LIGUE 1

Caen             vs   Marseille
Bastia          vs   Lorient
Evian T G   vs   Metz
Nice              vs   Montpellier
Rennes        vs   Lens

Alhamisi, 2 Oktoba 2014

ARSENAL BILA KUPEPESA MACHO WAPELEKA MSIBA MZITO UTURUKI.



WASHIKA,bunduki wa Jiji la Kaskazini mwa London timu ya Arsenal kuamkia usiku wa Ulaya jana wamefanya mauaji makubwa dhidi ya wahuni wa Uturuki timu ya Galatasaray kwa kuwafunga magoli manne kwa moja.

 Iliwachukua dakika ya ishirini na mbili kipindi cha kwanza mshambuliaji hatari aliye sajiliwa  katika  dakika za majeruhi toka kwa wapinzani wao Manchester United Dany Welback aliipatia goli la kwa baada ya kupokea pasi zuri toka kwa Alexis Sanchez ,dakika 30 aliweka nyavuni goli la pili safari hii akiwahi pasi ya Mesut Ozil kabla ya kwenda mapumziko Alexis Sanchez alihitimisha goli la tatu.

Kipindi cha pili kilianza kwa kushambuliana kwa zamu huku wageni wakitafuta kurejesha magoli yote waliofungwa kipindi cha kwanza dakika ya hamsini Welback aliandika hat trick yake ya kwanza akiwa na Arsenal na pia ni goli lake la nne tangu ajiunge na timu hiyo.

Mshambuliaji huyo aliyekuwa mwiba kwa kuisumbua ngome ya wapinzani hao huku Felipe Melo akizungushwa na Sanchez pamoja  mabeki wake dakika ya 69 washika bunduki hao walipata pigo baada ya mlinda mlango Szczesny kupata kandi nyekundu kwa kosa la kumdaka mshambuliaji  wa Galatasaray.

Jumatano, 1 Oktoba 2014

ARSENAL NA MAJERUHI KUWAVAA WATURUKI LEO HII

PATASHIKA ya ligi ya mabingwa kuendelea leo hii baada ya kushudia vigogo toka Hispania timu ya Barcelona wakichezea kichapo cha magoli matatu toka kwa mabingwa wa Ufaransa timu ya Paris Saint Germain, Chelsea, Bayern Munich,wakipata ushindi wa ugenini na pia Manchester City wameendelea kuchechemea baada ya kulazimishwa sare na Roma toka Italia.

Je nani kuibeba Arsenal kwani kila siku majeruhi wanaongezeka baada ya kuona viungo wa timu hiyo kama Mikel Arteta, Aron Ramsey, Jack Wilshere watakosa mechi ya leo dhidi ya timu ya Galatasaray toka nchini Uturuki.Hivyo jukumu la kiungo mkabaji itawategemea Flamini, Diaby,Rosicky nani ataanza katika kikosi cha kwanza.


Hivyo kutakuwa na mabadiliko kwani namba nane atasimama Alex Oxlade-Chamberlain kulia na kushoto Mesut Ozil na Alexis Sanchez wataongoza kutoa pasi kwa Santi Cazorla na Dany Welbeck huu utakuwa mtihani mgumu kwa Asener Wenger kwani mwishoni mwa wiki atakuwa ugenini kupepetana na watoto wa kupaki basi Chelsea ambao mpaka sasa hawajafungwa katika ligi ya England .

Mechi nyingine
Atletico Madrid vs Juventus,
Fc Basel             vs Liverpool
Malmo               vs  Real Madrid


Jumanne, 30 Septemba 2014

HAPATOSHI LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA LEO JUMANNE

KIVUMBI kuendelea tena leo na kesho katika ligi ya mabingwa makundi mbalimbali kujaribu bahati zao na kutumia vizuri viwanja vya  nyumbani, mechi ya mapema itaanza majira ya saa moja usiku katika jiji la Moscow nchin Urusi kati ya mabingwa CSKA MOSCOW watavaana na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich.

Majira ya saa tatu na dakika arobaini na tano usiku makundi ya E na H yatawasha moto wakati wenyeji Manchester City wanawakarisha wageni As Roma toka Italia.

Macho na masikio yatakuwa kundi F katika jiji la Paris nchini Ufaransa mabingwa wa ligi hiyo Paris Saint Germain watakuwa wenyeji wa Fc Barcelona toka nchini Hispania kwani timu hizo zimekuwa na upinzani mkubwa kwani hata msimu uliopita  zilikuwa kundi moja ambapo mechi ya kwanza zilitoka sare na ziliporejeana Barcelona walishinda.
  Pia kutakuwa na mechi nyingine katika kundi hilo Apoel Nicosia na Ajax watavaana.

Vijana wa kupaki basi watakuwa nchini Ureno watakumbana na wenyeji  Sporting Lisbon timu ambayo haijafungwa katika mechi zake za ligi sawa na Chelsea nao hawajafungwa katika ligi ya England na Schalke 04 watawapokea Maribor katika kundi hilo la G.

Hitimisho la leo kundi H, Bate Borisov na Athletic Bilbao pamoja na Shakhtar Donetsk vs Fc Porto.

Jumatatu, 29 Septemba 2014

MZIMU WA MSOTI WAENDELEA KUITESA SIMBA

TIMU ya Simba imeendelea kupata sare ya pili mfululizo katika mechi za ligi ya Vodacom Tanzania Bara huku tukiona uwezo wa kila mchezaji anayepata nafasi katika kikosi cha kwanza kati ya wachezaji wote waliosajiliwa na timu hiyo.

Licha ya kuwa na wachezaji wenye viwango vya kimatifa na wenye uzoefu katika mashindano mbalimbali hatujaona makali yao kama vile, kurejea kwa kiungo mkabaji Jonas Mkude hatujaona msaada mkubwa kuwalinda mabeki wake kwani timu hiyo inakosa pumzi katika kipindi cha pili.

Tatizo kubwa ambalo ni changamoto kwa kocha Patriki Phiri na bechi lake la ufundi ni sehemu ya mabeki wake kwani kumekuwa hakuna uwiano mzuri kati ya beki wa mwisho na wa nyuma bado kuna leta shida sana katika ukabaji wake,je nani tumlaum kocha aliyemuacha Donald Musoti ama kamati ya usajili iliyoamua kumsajili Emanueli Okwi?

Kwa upande wangu mzimu wa Musoti utaendelea kuitesa timu hiyo, kwani  ndio alikuwa nguzo imara katika ulinzi akisaidiana na Josefu Owino katika msimu uliopita, ushirikiano wao ulionekana hasa kwenye mechi ya mtani jembe walivyoweza kuwadhibiti washambuliaji wa timu ya Yanga

 Je kulikuwa na haja gani ya kumuacha beki kisiki na kuamua kumrudisha Okwi? ama ndio soka la Usimba na Uyanga wa kukomoana katika suala zima la usajili, wa timu hizi mbili zenye washabiki wengi nchini,ama siasa nyingi na majingambo mengi ambayo hayasaidii katika kujenga timu.

Musoti ni beki wa kimataifa na ana uwezo mkubwa sana katika ukabaji leo hii anaachwa na hatukuona nafasi yake anasajiliwa beki mzoefu  kwa lengo la kuziba nafasi yake. Isihaka bado hajawa na uzoefu katika mikikimiki ya mechi mbalimbali, wadau wengi bado wanajiuliza maswali je ni kocha hakuridhika na kiwango cha mchezaji huyo ama kamati ya usajili kwa ajili ya kufurahisha mashabiki wake na uongozi mpya uliopo sasa?


Ijumaa, 26 Septemba 2014

NANI KUNUNA AMA KUCHEKA WIKIEDI HII MECHI MBALIMBALI BARANI ULAYA?

WIKI hii kuna mechi katika ligi mbalimbali tazama ratiba

LIGI YA ENGLAND

Jumamosi;27
Liverpool               vs       Everton
Chersea                 vs      Aston Villa
Crystal Place          vs      Leicester City
Hull City                 vs     Manchester City
Manchester United  vs  West Ham United
Southampton           vs      Queens Park Rangers
Sunderland               vs     Swansea  City
Arsenal                     vs     Tottenham Hostspur

Jumapili ;28
West Bronwich Albion   vs  Burnely

SERIE A
Jumamosi;27

  Roma           vs            Hellas Veron
  Atalanta        vs           Juventus

Jumapili;28
  Sasoulo             vs        Ssc Napoll
  Cesena              vs         Ac Milan 
 Chievo Veron      vs       Empoll
Inter Milan            vs      Cagllari
Torino                   vs         Fiorentina
Genoa                   vs     Sampdoria

HISPANIA; LIGA BBVA
Ijumaa ;26

Elche     vs   Celta Vigo

Jumamosi;27

Villarreal             vs    Real Madrid
Barcelona           vs    Granada
Athletic Bilbao    vs     Eibar
Atletico Madrid  vs     Sevilla
Levante              vs     Rayo Vallecano

Jumapili;28
Getafe                              vs    Malaga
Deportivo la Coruna         vs     Almeria
Real Sociedad                  vs   Valencia
Cordoba                           vs    Espanyol

UJERUMAN;BUNDESLIGA
Ijumaa;26
Mainz 05     vs    Hoffenham

Jumamosi;27
Fc Cologne            vs          Bayen Munich
Freiburg                 vs          Bayen Leverkusen
Paderborn              vs          Borusia Monchengladbach
Schake 04             vs           Borusia Dotmund
Vfb Sstuttgat          vs           Hannover 96
Wolfsburg              vs           Werder Bremen

Jumapili;28
Augsburg      vs    Hertha Berlin
Hamburger    vs    Eintractfut

UFARANCE;LIGUE 1
 Jumamosi;27
Monaco         vs    Nice
Toulouse         vs    Paris Saint Germain
Lille                vs      Bastia
Lorient            vs    Evian Thonon Gaillard
Metz               vs    Reims
Montpellier      vs  Guingamp

Jumapili;28
Bordeaux      vs    Rennes
Lens              vs   Caen
Nantes           vs   Lyon
Marselle         vs   Saint Etienne

URENO;LIGA ZON SAGRES

Ijumaa;26
Sporting Cp            vs              Fc Port

Jumamosi;27
Estoril            vs                   Benfica
Braga             vs                   Rio Ave


Alhamisi, 25 Septemba 2014

SIMBA YAANDAMWA NA MAJERUHI

KLABU ya simba imeendelea kuandamwa na majeruhi  kuelekea kwenye mchezo wake dhidi ya Polisi Morogoro utakaofanyika Jumamosi hii katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salam majira ya saa kumi jioni.

Miongoni mwa wachezaji wa timu hiyo ambao wamepata majeruhi ni Issa Rashid ''Baba ubaya'', Paulo Kiongera, Abdi Banda, Nassor Masoud chollo  pamoja na mlinda mlango namba moja Ivo Mapunda.

Licha ya kuwa na majeruhi mengi hatutaraji kuona mapungufu mengi katika timu hiyo kwani ina wachezaji wengi wenye uwezo wa kuziba mapengo hayo, hivyo jukumu kubwa linabaki kwa kocha wa timu hiyo pamoja benchi zima la ufundi kushauriana nani acheze katika nafasi hizo.

Tuliona katika mechi ya ufunguzi timu hiyo ilivyopoteza nafasi nyingi katika sehemu la umaliziaji kwani walikosa nafasi nyingi za kufunga magoli licha ya kuwa na safu hatari ya wafungaji huku ikiongozwa na mfungaji bora wa msimu uliopita Hamis Tambwe raia wa Burundi.

Habari njema kwa mashabiki klabu hiyo ni kurejea kwa kiungo mkabaji Jonas Mkunde aliye kuwa kwenye majeruhi kwa muda mrefu aliyopata akiwa katika kambi ya timu ya Taifa, hivyo ataongeza nguvu katika eneo la kati huku akisaidiana na mabeki wake.

Kwani katika mchezo uliopita tuliona mapungufu katika kiungo mkabaji hasa katika kipindi cha pili mpaka ikapelekea wapinzani kusawazisha magoli yote mawili licha ya kuongoza kipindi cha kwanza.

Jumatano, 24 Septemba 2014

TAZAMA YALIYOJILI LIGI MBALIMBALI KATIKATI YA WIKI HII

Michezo mbalimbali imechezwa wiki hii kutoka ligi tofauti tukianzia;

ENGLAND; CAPITAL ONE

Arsenal             1-2   Southampton
Cardiff city       0-3   B'mouth
Derby county   2-0  Reading
MK Dons         2-0   Bradford
Swansea           3-0  Everton
Sunderland       1-2  Stoke city
Leyton              0-1  Sheffield
Liverpool         2-2  Mid'brough

Shrewsbury     1-0   Norwich city
Fulham            2-1   Doncaster

HISPANIA :LA LIGA

Real Madrid   5-1 Elche
Celta Vigo      2-1 Diportivo la Coruna

ITALIA:  SERIE A

Empoll    2-2   Ac Millan

UJERUMANI: BUNDESLIGA

Bayern munich    4-0 Paderborn
Eintr. Frankfurt    2-2 Mainz 05
Hoffenheim         3-3 Freiburg
Werder Bremen   0-3 Schalke 04

 UFARANSA:  LIGUE 1

Reims         0-5 Marselile
Rennes       0-3 Toulouse

Jumatatu, 22 Septemba 2014

ANGALIA RATIBA YA KOMBE LA LIGI UINGEREZA 'CAPITAL ONE'


Jumanne 23:saa 3:45 usiku

Arsenal       vs    Southmpton
Cardiff        vs    B' mouth
Derby          vs   Reading
Mk Dons     vs   Bradford
Swansea       vs  Everton
Sunderland   vs  Stoke City
Leyton          vs  Sheffield
Liverpool      vs  Mid'brough
Shrewsbury   vs  Norwich city
Fulham          vs   Doncaster

RATIBA ZA LIGI YA BUNDESLIGA,SERIA A NA LALIGA KWA WIKI HII

BUNDESLIGA

Jumanne 23:
Bayern Munich        vs    Paderborn
Eintrach Frankfurt    vs   Mainz 05
Hoffenheim               vs   Freiburg
Werder Bremen         vs   Schalk 04

Jumatano 24:
Bayer Leverkusen                 vs  Augsburg
Borrusi Dortmund                 vs  Vfb Stuttgat
Borrusia monchengladbach   vs  Hamburger sv
Hannover 96vs                       vs  Fc cologne
Hertha Berlin                         vs  Wolfsburg

LA LIGA

Jumatatu 22:
Getafe        vs    Valencia

Jumanne 23:
 Real Madrid    vs  Elche
Celta vigo         vs  Deportivo la coruna

Jumatano 24:
Almeria             vs  Atletico Madrid
Eibar                  vs  Villarreal
Rayo vallecano  vs  Athletic Bilbao
Granad                vs  Levante
Malaga                vs  Barcelona
Sevilla                 vs  Real sociedad

SERIA A

Jumanne 23:
Empoll       vs  Ac millan

Jumatano 24:
Calgllarl          vs    Torino
Fiorentina        vs   Sassuolo
Hellas verona   vs   Genoa
Inter millan       vs  Atalanta
Juventus            vs   Cesena
Parma                vs   Roma
Ssc Napoll          vs  Palermo
Sampdoria           vs Chievo verona

Alhamis 25:
Lazio         vs     Udenese